Ujasiri ni mali.Hvy kijana jiajiri hujachelewa.Kuwa mjasiriamali siyo kazi sana endapo utajitambua na kujiamini lkn pia kuamua kuwa mjasiriamali.
Leo nikuhabarishe kuhusu utengenezaji wa viatu vya ngozi hasa vile viatu vya kimasai.Viatu hivi vinauzika sana tena kiurahisi kutokana na mahitaji yake kuwa makubwa sana kwa jamii inayotuzunguka lkn pia ni bidhaa isiyo ya msimu ama mpito kama ilivyo aina nyingine ya viatu.Biashsra hii inahitaji mtaji mdogo sana ukilinganisha na biashara ya duka.Biashara hii ukiwa na Tsh.250,000/= tu unajikuta una kiwanda chako mwenyewe na ukajitengenezea pesa.Ili kuanza biashara hii vifuatavyo vinahitajika:-
(1)Ngozi nyeusi.
(2)Box
(3)Shwapa
(4)Gundi
(5)Valvet
(6)Bomba
(7)Soli
(8)Mashine ya ku-shape kiatu chako.
Vitu hivi vyote vipo ktk maduka ya ujasiriamali mikoani kote ambapo vitu vingine tajwa hapo juu hugharimu Tsh.89,000/=tu,na mashine ya umeme hugharimu Tsh.150,000/=tu.Na gharama hizi tumechukulia kutokana na kwamba ndo unaamza kwa mara ya kwanza lkn gharama hupungua kutokana na baadhi ya vitu kutokana na kwamba baadhi ya vitu hudumu kwa muda kama vile gundi au mashine hivi huchukuwa muda kuisha ama kuhsribika hivyo ukinunua mara moja unaweza usinunue tena kwa haraka.
Kwa leo tuishie hapa lkn zaidi endelea kutufuatilia ili kujifunza zaidi kuhusu fursa hii adhimu na yenye kipato kikubwa.Au tupigie +255-629108340/+255-629114323/+255-62588
Whatsapp +255-629108340
Instagram:@joachimmkwawa.
7699.
Whatsapp 0629108340
Maoni 5 :
I like it.
And I like to learn more about this.So am here for this.
Naitwa James, hivi ni WAPI naweza kupata pande la ngozi kwa bei rahisi, lakini pia nawezaje kupata duka la vifa vya ngozi kwa tafadhali.
naomba kupewa jina la mashine ya kushape viatu,,tafadhari
Nimekubali asee
VIP naweza pata darasa la kutengeneza hvo viatu?
Chapisha Maoni