JIFUNZE KUTENGENEZA SABUNI YA KUFULIA YA MAJI.
Leo tena bado tupo hapa kukuhamasisha na kukufunza namna ya kujiajiri wewe mwenyewe.Jifunze tena Fursa hii adhimu.
Sabuni hii ya maji unawezaitumia kwa kudekia sakafu yako,kufulia ama kuoshea vyombo vyako nyumbani.
(1)MAANDALIZI.
(a)Beseni kubwa au Diaba.
(b)kijiko.
(c)Mwiko.
(2)MAHITAJI/MALIGHAFI.
(a)Salphonic acid nusu Lita.
(b)Sless robo Lita
(c)Sodash robo kilo.
(d)Maji Lita 15.
(e)Rangi nusu kijiko.
(f)Sodium salfet nusu kilo
(g)Perfume vijiko 2.
(h)Formaline vijiko 2
(j)Glyceline vijiko 4.
(3)JINSI YA KUTENGENEZA.
(a)Andaa Diaba(jaba)au chombo chochote mfano beseni lenye ujazo wa Lita 20.
(b)Weka maji kwenye chombo hicho na hakikisha chombo chako ni kikubwa kuzidi wingi wa maji yako.
(c)Weka sulphonic acid,sless vyote kama ulivyoelekezwa na kuvipima kwa vipimo tajwa hapo juu.Vichanganye kupata mkorogo ama mchanganyiko mmoja bila kuukoroga lakini ukiwa undani ya jaba lako.
Tia maji yote Lita 15 kwenye jaba na uanze kukoroga kuelekea upande mmoja yaani kama unakoroga kuelekea kulia usigeuze kuelekea kushoto.
(d)Weka sodash,Rangi uipendayo iwe bluewax,greenwax ama redwax.Tia perfume,Formaline na Glyceline kisha endelea kukoroga mchanganyiko huo kwa dakika 2 au 3.
(e)Chukua chombo kingine cha plastic mfano jagi au bakuli kisha chota huo mchanganyiko wako kiasi halafu utie sodium kwenye bakuli au jagi hilo na ukoroge vizuri.
(f)Kisha mimina mkorogo huo wa kwenye bakuli au jagi kwenye ule mchanganyiko wako wa awali uliyopo kwenye jaba na endelea kukoroga na hapo utaona mchanganyiko unaanza kupanda juu.Hii ina maana kwamba Sodium huingeza wingi wa sabuni yako.
Hivyo ukikoroga Lita 15 hakikisha chombo chako kina ujazo wa Lita 20 au zaidi.
Na Formaline husaidia kuitunza sabuni yako isiharibike haraka yaani ukiweka formaline basi sabuni yako yaweza kaa hata mwaka 1 bila kuharibika.
Baada ya hapo yaani umemaliza kutengeneza chukua sabuni yako na mimina katika vifungashio ulivyokwisha kuviaandaa,weka lebo yako.Na tayari sabuni yako itakuwa tayari kwa matumizi ama biashara.
Na hii itakuwa ni sabuni safi,nzuri,yenye kunukia,raini isiyochubua mikono ama kufubaza nguo na itakayokuoa matikeo mazuri kwako na sikoni.
Kumbuka.
Zipo aina 5 za Formaline hivyo kuwa makini pindi unapokwenda kununua malighafi zako dukani.Na malighafi hizi hupatikana kwenye maduka maalum ya ujasiriamali tu na vinginevyo.
Aina za Formaline
(1)Formaline ya chakula
(2)Formaline ya kutunzia dawa
(3)Formaline ya kutunzia sabuni
(4)Formaline ya kutunzia maiti
(5)Formaline ya kuzuia wadudu wasiharibu lotion(losheni).
Ahsante sana naomba niishie hapa kwa Leo.
Kesho tena usisite kutufuatilia ili kujuwa tumekuletea kitu gani cha kujifunza kutengeneza na kukufanya ukajiajiri wewe mwenyewe ukajiingizia kipato..
Piga +255625887699
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni