Ijumaa, 18 Septemba 2020

BREAKING NEWS:-SERIKALI YATANGAZA NAFASI MPYA ZA AJIRA NEEC

Kwa mara nyingine tena Serikali ya Tanzania imetangaza nafasi zingine mpya za ajira.
Bofya hapa>>https://www.kijiwe.co.tz/2020/09/employment-opportunities-at-national.html?m=1

Jumamosi, 23 Mei 2020

MTOTO ALIYETUPWA KWENYE SHIMO LA CHOO WILAYANI NGARA MKOANI KAGERA AOKOLEWA NA JESHI LA ZIMAMOTO.

Ngara Kagera;
Mtoto wa mwaka mmoja aliyetupwa kwenye shimo La Choo cha wasichana shule ya msingi wilayani Ngara mkoani Kagera hatimaye ameokolewa.
Oparesheni hiyo ya uokozi ilifanywa kikamilifu na kufanikishwa kwa Ufanisi mkubwa wa Jeshi La Zimamoto na Uokoaji nchini Tanzania.Jeshi La Zimamoto nchini baada ya kupokea taarifa za tukio hilo La kusikitisha lilifika haraka eneo La tukio na kuanza kazi ya uokoaji mara moja na kufanikiwa kunusuru uhai wa mtoto huyo kwa kumtoa ndani ya shimo kupitia chemba(mfuniko)wa kalo La choo hicho.
Askari wa Jeshi La Zimamoto Constable Denis Minja alizama shimoni humo kwa kamba na kwa ujasiri na ufanisi mkubwa akiongozwa na Jeshi hilo alifanikiwa kumuokoa mtoto huyo ambaye kwa kipindi chote alisikika akilia ndani ya shimo hilo.
Kwa ujasiri huo pekee na wa kizalendo hatimaye Kamishina Jenerali wa Jeshi La Zimamoto na Uokoaji nchini Ndugu John Masunga akaamua kumpandisha cheo askari Denis Minja kutoka kuwa Constable hadi cheo cha Koplo.
Sisi kama jamii kwanza tunalipongeza Jeshi letu La Zimamoto na Uokoaji nchini kwa kutimiza vema wajibu wao wa kizalendo katika kushugulikia jambo hilo.Lakini pia tunalaani vitendo viovu na vya kinyama kama hivi vya watu(wazazi/walezi)kuchukua sheria mkononi na kutekeleza matukio yasiyo ya kibinadamu kama haya.Sambamba na kuwaasa Watanzania kuwa na hofu ya Mungu na kwamba ni kosa kisheria kutishia ama kukatisha uhai wa wengine kinyume na sheria zetu nzuri na bora zinazompa Mtanzania Uhuru na haki ya kuishi kwani kwa kufanyaje hivyo ni kupoteza nguvu kazi ya kesho kwa Jamii na Taifa kwa ujumla.

Jumamosi, 16 Mei 2020

HIZI HAPA FURSA 5 ZA KIBIASHARA ZINAZOHITAJI MTAJI MDOGO

Habar za wakati huu ndugu msomaji,mjasiriamali na maana jukwaa mwenzangu wa jukwaa pendwa la UJASIRI NI MALI(JIAJIIRI).
Hongera sana kwa mfungo wa Ramadhan,hongera kwa mapambano dhidi ya Covid-19.Na lakini pia hongera kwa kuendelea kuchakalika kimaisha ukiwa nyumbani.
Najuwa kila mtu anapambana katika shughuli mbalimbali ili kujipatia kipato.Yamkini unajiuliza leo mimi na jopo langu tumekuletea nini mezani??.
Basi leo kama kawaida yetu tunapenda kukuona wewe mjasiriamali ukiwa juu kibiashara na kipato.
Leo tumekusogezea fursa 5 muhimu za kibiashara ambazo zinahitaji mitaji midogo sana ili kuzianzisha/kuzifanya.
Angalia video hii mwanzo hadi mwisho naamini utajifunza zaidi.
Usisite kuja YouTube channel yetu iitwayo Mnyausi TV ili upate video mbalimbali za mjasiriamali.SUBSCRIBE Channel yetu(Mnyausi TV),Like,Comment na ku Share.
By
Joachim Mkwawa.


Ijumaa, 24 Aprili 2020

MBUNGE DEVOTHA MINJA APAMBANA NA CORONA MOROGORO

Mbunge wa Vitu maalum Morogoro mjini kupitia CHADEMA Mh.Devotha Minja;hii Leo amesaidia Wananchi mbalimbali wa Kata 15 za Manispaa ya Morogoro kwa kuingia mitaani na kugawa Barakoa 5000 kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya COVID-19.
Barakoa hizo zimegawiwa kwa makundi mbalimbali wakiwemo walemavu,mama ntilie,bodaboda,madeleva na makondakta wa daladala,wasari na watu mbalimbali wakubwa kwa Wagogo lengo likiwa ni kuonesha kwa vitendo juhudi zake katika kuhakikisha Wananchi wanajikinga na kuwa salama dhidi ya Corona ugonjwa ambao umekuwa tishio kwa afya uhai wa binadamu.






JIFUNZE KUTENGENEZA BARAKOA(MASK),COVID-19 INAUA.

Habari mpendwa msomaji wetu wa blog hii pendwa.
Natumai umzima wa afya lakini hongera kwa mapambano dhidi ya CORONA maana hili ni janga kubwa linalotutesa Duniani kote.
Leo mjasiriamali mwenzangu naomba nikushirikishe na kukuhamasisha kuhusu fursa iliyopo kutoka na janga hili(COVID-19).
Fursa hii itakuwa ni msaada kwanza kwako wewe mwenyewe lkn pia kwa familia na jamii inayokuzunguka kwa ujumla.
Unaweza kuwekeza Tsh.30'000/=(Elfu thelathini) na lakini ikakufanya kuingiza kipato mara 2 hadi 3 ya pesa uliyoiwekeza kila siku.Fanya hivi ingia dukani nunua kitambaa na lactic kisha mptafute fundi mzuri wa kushona Mpe akutengenezee barakoa(mask)kisha ingia Nazi masokoni,stendi za mabasi,au hata majumbani na uziuze kwa bei rafiki kwa mteja.Hapo utasidia jamii kujikinga na CORONA lakini pia utapata kipato.
Lakini hapa nimekuwekea video ya namna/jinsi rahisi ya kutengeneza barakoa za aina mbalimbali.

NGOMA ASILI:WAGOGO KUTOKA DODOMA TANZANIA.

Leo tunakusogea ngoma ya Asili kutoka kwa Kabila La Wagogo lenye maskani yake jijini Dodoma.Kwa kawaida ngoma hii huchezwa wakati kiangazi baada ya mavuno.Yaani nyakati za mapumziko baada ya kipindi kirefu cha kilimo kumalizika.Lakini pia ngoma hii huchezwa wakati wa sherehe mbalimbali za kawaida,Kiserikali na kimila.
Karibu ufurahie.
Ngoma hii huitwa "Mheme".
Na hiki ni kikundi cha ngoma Asili kiitwacho Nyota kutoka kijijini Majeleko,wilaya ya Chamwino jijini Dodoma.
Mimi ni Joachim Mkwawa.

Jumatatu, 20 Aprili 2020

VISA 84 VIPYA VYA COVID-19 VYARIPOTIWA TANZANIA HII LEO.

Wizara ya Afya nchini Tanzania yatangaza visa vipya 84 vya Corona.Na hivyo kufanya kufikia visa 254 tangu kuripotiwa kwa mara ya kwanza kuwepo kwa maambukizi ya Corona nchini.
Wananchi wote wameendelea kukumbushwa kuchukua tahadhari kama inavyoshauriwa na Wataalam wa Afya ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huu hatari.Tahadhari hizo ni pamoja na kunawa mikono kwa maji safi na sabuni maalumu kila mara,kuvaa barakoa,kuepuka misongamano na mikusanyiko isiyo ya lazima nk.


VITUKO VYA CORONA:KAMANDA AKAGUA GWARIDE

Covid-19 imeleta vituko ambavyo ni darasa la kujifunza.Kila mmoja hivi sasa anajaribu kubuni njia sahihi atakayoitumia kuelimisha jamii inayomzunguka kuhusu janga la Corona linaloiendesha Dunia hivi sasa.Tizama video hii Kamanda akikagua GWARIDE la Corona.

MANENO YA MWISHO YA MCH.GEDTRUDE RWAKATARE

Haya ndiyo maneno yake ya mwisho marehemu Asikofu Mama Gertrude Rwakatare alipohubiri ibadani.Na hapa anazungumzia kuhusu Covid-19 sambamba na magonjwa mengine ya milipuko(Tauni) kama yalivyotabiriwa kwenye kitabu kitakatifu(Biblia).Mama Gertrude Rwakatare alikuwa Askofu wa kabisa la Mlima wa Moto la jijini Dar es Salaam.
Askofu Rwakatare amekutwa na umauti alfajiri ya leo akiwa Hospitali ya Mloganzila alipokuwa akipatiwa matibabu.Tutakukumbuka sana mama yetu hasa kwa huduma yako bila kusahau ule"UPEPO WA KISULISULI".
Mungu akulaze pahala pema,Amen.

VITUKO VYA CORONA:WAUMINI WARUSHIWA MEZA YA BWANA.

Corona imefanya tunashuhudia vituko vingi sana Duniani kote.
Hats hivyo vituko hivi vimekuwa msaada sana katika kuifunza jamii namna ya kujikinga ama kuepuka maambukizi mapya ya Covid-19.
Hebu tazama video hii.

Jumamosi, 18 Aprili 2020

MAFURIKO YASABABISHA MAAFA UVIRA NCHINI CONGO

Hali bado ni tete ama mbaya tarafa ya Uvira;huko nchini Congo.Baada ya miili ya watu kupatikana ikiwa imetapakaa mitaani.Hali hii imekuja baada ya maji yaliyotokana na mafuriko kuanza kupungua.
Miili ya watu zaidi ya 30 imeopolewa ikiwemo ya watoto wachanga.
Wakazi wa tarafa hii ya Uvira wameiomba serikali na Rais wa Congo kuwahi kupeleka misaada ya kibinadamu kabla ya magonjwa ya milipuko kuanza kutokea.
  Kutokana na jiografia na ukubwa wa nchi ya Congo pamoja na hali ya miundombinu ya eneo hilo bado Serikali haijafika Uvira kutoka Kinshasa.
Watu zaidi ya laki moja mjini Uvira hawana makazi wala Chakula.





MWANGA WA AJABU ULIVYOTOKEA NA KUSHANGAZA WATU KARIAKOO NCHINI TANZANIA

Juzi siku ya jumatano mitaa ya Kariakoo jijini Dar es Salaam nchini Tanzania kulitokea hali ya ajabu na ya kushangaza ambapo kulitokea ishara za ajabu na kushangaza zilizotanda barabara kwenye anga La jiji hilo huku hali hiyo ikiwaacha watu katika mshangao wa aina yake.
Wadau na watu mbalimbali kwa imani zao walitolea ufafanuzi/utabiri juu ya halo hiyo.

Ijumaa, 17 Aprili 2020

KENYA:-WADAU WALALAMIKIA UNYANYASWAJI WA WATU WEUSI NCHINI CHINA.

Watu,wadau na Viongozi mbalimbali kutoka ukanda wa Afrika ya Mashariki wameendekea kulamikia na kulaani vikali juu ya vitendo visivyo vya kibinadamu wanavyofanyiwa Waafrika nchini China.
Ungana nami kwenye hii video.

HATUA 6 MUHIMU KATIKA MAISHA YA MWANADAMU

KUTOKA IBADANI.
Habari ndugu msomaji na mfuatiliaji wetu wa blog hii pendwa.
Tunatumai umzima wa afya.Awali ya yote tunatoa salamu za pole kwa wagonjwa wote wa COVID-19 Ulimwenguni kote,Pia pole kwa viongozi na wafiwa wote Duniani kutokana visa na vifo vitokanavyo na janga hili la Corona.Hata hivyo tunachukua fursa hii kuwakumbusha watu wote kuchukua hatua na tahadhali mbalimbali katika kujikinga na maambukizi ya ugonjwa juu hatari.Aidha tunawakumbusha kila mmoja wetu kuchukua hatua ya kuelimisha wengine kuhusu COVID-19 na namna ya kujikinga na zaidi sana tunashauri tubaki majumbani tukiwa salama.
   Mpya hii Leo ni kwamba kuanzia Leo Mnyausiblog tutaanza kukuletea makala za mafundisho Kutoka Ibadani kupitia watumishi mbalimbali wa Mungu wanaohudumu makanisani na misikitini.
Lengo la safi hii ni kukuelimisha na kukuburudisha zaidi na zaidi.
Ni furaha na wajibu kwetu kukuona unaelimika na kukua kiungu(kiimani)na maisha kiujumla.
Leo tunaye Mchungaji Peter Mitimingi kutoka Tanzania akiwa na somo la
HATUA 6 MUHIMU ANAZOZIPITIA MWANADAMU KATIKA MAISHA.
Karibu ujifunze.

Alhamisi, 9 Aprili 2020

SONGA MBELE USIRUDI NYUMA.

Yeah!!;
Ya mkini kuna mambo unayapitia ni magumu sana kwako,unaona ni mtihani mkubwa sana kwako kuufauru.Ama yawezekana uko na maumivu makali sana yanayoutesa moyo wako.Umefukuzwa kazi,unatafuta kazi hupati,umetengwa,umefeli mitihani,unaugua ama unauguza.Umepoteza wapendwa wako,tumaini la maisha hulioni na unahisi kunyanyasika sana moyoni mwako na mengineyo kama hayo;Basi ndugu yangu ninakusihi kwamba usife moyo kwa sababu changamoto kamwe huwa hazikimbiwi.Changamoto zipo ili kutufanya tujijenge na kwa bora zaidi Kule tuendako.
Kamwe huwezi toka darasa moja kwenda kingine ikiwa hukuufauru mtihani.Unayoyapitia Leo ni mtihani tu.Usikate tamaa,nyanyuka usonge MBELE.Simama uendelee na safari;ushindi wako upo.SONGA MBELE USIKATE TAMAA.
Joachim Mkwawa
Motivational Sleeker
mnyausiblog.blogspot.com

Jumanne, 7 Aprili 2020

KUPIGWA TUNAJITAKIA

Leo sina maneno mengi sana kueleza.Lakini kifuatacho kinajieleza wazi kabisa ya kwamba mambo mengine huwa tunajitakia.
Ndiyo!;Kupigwa Tunajitakia.
Joachim Mkwawa.
mnyausiblog.blogspot.com

Jumamosi, 4 Aprili 2020

JINSI YA KUANZISHA BIASHARA

Joachim Mkwawa & Noa Ubongo.

Hello
Team wachapakazi,wapambanaji,wachakalikaji na wazee wote wa mihanjo mjini.
Natumai site tuko poa kabisa.
Najuwa kila mmoja wetu yuko na ndoto za kumiliki biashara yake mwenyewe si ndiyo??.
Basi kama kawaida yangu Mnyausi nipo hapa kukusogezea nondo mbalimbali za kukuvusha pindi unaiendea hatima yako maishani.Hii ni Mnyausiblog na chombo kwa hewa hivi sasa ni UJASIRI NI MALI(JIAJIRI),huku mada mezani ikisomeka kama:-

JINSI YA KUANZISHA BIASHARA.
Vipo vingi vya muhimu kujifunza na kuvijuwa kabla ya kuanzisha biashara.
Yamkini waweza kuwa tayari ulikwisha wahi kujaribu kuanzisha biashara ikafa ama bado inaendelea nk;lakini leo nimekusogezea maarifa zaidi yatakayo kuongezea fahamu na kufanikiwa kibiashara.Darasa hili pia unalipata YouTube channel yetu jina Joachim Mkwawa,hakikisha una subscribe na ubonyeze kengere nyekundu ili uwe wa kwanza kupata videos mbalimbali za mafunzo tunazoziweka humor.
Mimi ni;
Joachim Leonard Mkwawa
Motivational Speaker
mnyausiblog.blogspot.com

Ijumaa, 3 Aprili 2020

TIME TO RETHINK ABOUT LIFE.

With
Mr.Criss

Emptiness and Vanity!.
Our cars are just parked there,no where to go to.The private jets are lying in waste,air spaces are all shut,every country nursing its Citizens and fighting an unseentiny enemy.
Each man is confined to a room in those big mansions and the designer;clothes,bags,shoes,perfumes and make-up kits have all become useless and serving no purpose.
No more urgent appointments and business meetings that diprive us of time with our Creator and family.
No parties to attend and hangouts to meet up with friends,no more canvoys and sirens,even the money stocked away in the accounts and slack always are useless....

Even our expansive and expensive church auditoriums are empty,it is now each man with his Creator in truth and air to breathe,we just want to be alive.Nothing else is really important.
This World has never seen vanity as it is today!.

Good News is;we all have one more chance to introspect,to reflect and ask,"Why does my Creator need to keep me alive through this?,To marry or buy new cars or perhaps finish my doctorate or receive my blessings from professed men of God?".
What is my purpose in life now and after COVID-19?.
Why does my Creator need to spare me and allow others die?.
Of what value am I to humanity and to my Creator and His Kingdom that should make Him to spare me?.
Let us pray and change our ways and seek a more purposeful living after COVID-19.
May God help us to seek Him the more.
This too shall pass.
Joachim Leonard Mkwawa
Motivational Speaker
mnyausiblog.blogspot.com

Alhamisi, 2 Aprili 2020

JINSI YA KUBAKI KUWA MASIKINI(THREAD)

Na Joachim Mkwawa
Motivational Speaker.

Habari mwanadawati mwenzangu wa dawati hill la UJASIRI NI MALI(JIAJIRI).
Dawati ambalo kimsingi hukujenga na kukuhamasisha katika kujiajiri wewe mwenyewe ama kuwekeza hata kama upo katika ajira rasmi.
Dawati hill kipekee ndilo hupatikana na kutukutanisha wajasiriamali kupitia blog hii pendwa Duniani kote.Na Leo nimewiwa kukushirikisha hatua ama mambo muhimu ya kuzingatia ikiwa unataka KUBAKI KUWA MASIKINI MAISHANI MWAKO.

JINSI YA KUBAKI KUWA MASIKINI.
Yamkini unaweza usinielewe;lakini kufuatia hatua hizi naamini ukizifuata na kuzifanyia kazi kikamilifu hakika lazima ubaki kwenye umasiki.
(1)Kamwe usiamke mapema,Endelea kulala na kujinyoosha.We lala tu hadi jua litakapochomoza,yaan hakikisha unalala hadi uone mwanga wa ndani kwako unafana na wa nje.Au lala hadi njaa itakapokuuma ndipo uamke.
(2)Kamwe usipange namna sahihi ya kuitumia pesa yako.We zitumie tu utakavyo hasa pale unapozipata.Na zikiisha hata usipoteze muda kukaa chini na kufikiria ulizitumiaje.
(3)Kamwe usiwaze wala kufikiria ku-save pesa yako,subiri hadi upate pesa nyingi ndipo uanze ku-save.Uta-save vipi pesa yako wakati unazo kidogo!??.Tena wapuuze wale wote wanaokushauri ku-save kwani hawakutakii mema wewe na pesa yako.Watakupangiaje kutumia pesa yako ilihali hawakukusaidia kuitafuta??.
(4)Kamwe usijiingize kwenye biashara ambazo huwa mnaziita za kitoto tena ni za watu wasiyosoma.Wewe ni msomi bwana na tena umemaliza chuo kikuu,umeajiriwa na halafu unalipwa vizuri mshahara mkubwa.Sasa ya nini ufanye biashara za kuuza Viazi?,Utauzaje mbogamboga?,Yaani na usomi wako halafu ukauze viatu vya mtumba kweli?.We msomi bwana hupaswi kufanyaje biashara za watu wasiyosoma aisee.Wewe unafaa ukae tu ofisini upigwe na kiyoyozi Basi.Una shida gani kwani.
(5)Kamwe usifikirie kuanzisha biashara mpaka pale Malaika atakaposhuka kutoka Mbinguni akuletee mtaji mkubwa wa kuanzisha biashara.Kwa wakwambie uanzishe biashara hata kwa mtaji mdogo eti kisa wafanyabiashara wengine wakubwa kama akina MO au Bakhresa walianza kwa kuuza migahawa.Wewe ni smart bwana unatakiwa uanze na mamilioni.Sawa eeeh!??.
(6)We lalamika kuhusu kila kitu Ila Kamwe usilalamike kuhusu uvivu wako na Attitude yako.We ilaumu tu Serikali ya Magufuli kwamba imekaza vyuma,Lalamikia benki zisizotaka kukuamini na kukukopesha mtaji,laumu makampuni mbalimbali yaliyokunyima ajira ama yaliyokufuta kazi.Kwa sababu wote hao ni wabaya na hawataki wewe uwe tajiri.
(7)Tumia pesa nyingi kuliko kipato chako.Na ili kufanikisha hilo wewe tununua bidhaa kwa mkopo,azima pesa kwa rafiki zako,nunua samani nzuri za ndani,Nunua Brand New LG flat screen.Kopa pesa benki ama kazini kisha kanunue gari Kali na ya kisasa ya kutembelea.Honga vyovyote vile utakavyo hadi mjini wakukome.Ndiyo pesa si ni zako bwana;unakwama wapi?.
(8)Shindana katika kuvaa.Hakikisha hupitwi na fashion yoyote mpya ya nguo,viatu,gari na simu.Nunua kila aina ya simu inayotoka yaani usikubali kupitwa na Toledo jipya la simu;hata kama ulikuwa na Samsung Galaxy S6 uliyoinunua milioni 1 we iuze tu hata kwa laki 7 kisha ongezea pesa kiasi uende kununua Samsung Galaxy S7.Ndiyo kwa sababu hizo simu kalikali zimetengenezwa kwa ajili yako bwana.
(9)Ukishindwa kununua gari mpya,Nunua hata used lakini Kali na ambayo gharama zake kwenye kuihudumia ni mara 2 ya mshahara wako ama inayodumu muda mrefu.
(10)Halafu mwisho sawa wala usiogope maneno ya watu.Maana watu kama wewe msiyokuwa serious na maisha huwa hamzeeki wala nini.Endelea kuishi hivyo hivyo.
Fainali ni uzeeni.
Hivyo ajili za kuambiwa vema ukachanganya na za kwako.
Ukifanya kinyume na hizo hatua lazima utatajirika na ikiwa utazifuata na kuzitii vema hizo hatua Basi naamini umasikini utakuhusu.
Mimi ni
Joachim Leonard Mkwawa
Motivational Speaker
mnyausiblog.blogspot.com

Jumatano, 25 Machi 2020

TANGAZO:-NAFASI ZA KAZI.

Wanahitajika
(1)Mfamasia-Kuuza duka la dawa
(2)Mhudumu/Wakala-Huduma za kifedha(Tigopesa,M.pesa,Halopesa,Airtel money)


Vigezo:-
Mfamasia
~Cheti cha Nursing assistant
~Cheti cha Ado
~Cheti cha Form 4
~Umri kuanzia miaka 18-35
~Awe Mtanzania na aliye tayari kufanya Kazi bila kusimamiwa.

Mhudumu/Wakala
~Barua toka serikali ya Mtaa anakotoka.
~Uzoefu wa masuala ya mitandao ya simu.
~Awe Mtanzania na mkazi wa Dodoma.
Piga simu +255 653890025 au +255 626176465
NB:-
Usibip wala kutuma SMS hautajibiwa.

TANGAZO:NAFAZI ZA KAZI WIZARA YA AFYA

TANGAZO LA nafasi za kazi upande Udaktari.TANGAZO LA Wizara ya Afya.



Jumamosi, 21 Machi 2020

UMEME:-TANZANIA YAONGOZA AFRIKA KWA VIJIJI VYENYE UMEME.

Wizara ya Nishati nchini yathibitisha hilo.

Q.CHILA AFUNGUKA KUHUSU FA KUKUMBWA NA CORONA.

Msanii mkongwe wa Muziki wa Bongo fleva nchini Tanzania;Q Chila amesema kwamba kuhusu msanii mwenzake wa Muziki huo nchini Mwana FA kupatwa na Maambukizi ya Virusi vya CORONA inawezekana isiwe kweli Bali ni kiki tu.
Hutu hapa msanii Q'Chief ukipenda Q'Chila akifunguka.

Ijumaa, 20 Machi 2020

KUPIGWA TUNAJITAKIA

Hello team
Nimerejea na segment yetu ile toka kitambo.Hapa ndipo huwa tunanyoosha palipopinda.Ni makavu live tu.Haijalishi itakuuma kiasi gani.
Ujuwe mara nyingi KUPIGWA huwa hakuji tu hivihivi.KUPIGWA siyo lazima kweli MTU akushike na kuanza kukupiga kama wengineo mnavyofikiria;laa hasha.
Wakati mwingine kuibiwa Mali yako ni KUPIGWA,Kurogwa ni kupigwa pia.

Kujitakia ni pale ambapo Mtu unafahamu fika kwamba kufanyaje jambo Fulani hata kama halikukatazwa ni vibaya ama si kitendo cha kiungwana lakini cha ajabu kwa makusudi tu MTU anaamua kufanyaje buku unajuwa ni kosa kufanya hivyo.
Sasa mfano wewe mdada Mtu mzima na akili zako tens usikute unaishi na wazazi wako hasa mzazi wako wa kiume unaishi naye nyumba moja na Halafu bila woga kweli unapofua nguo zako za ndani na kuzianika nje tena umezisambaza kamba nzima ni sawa??.
Hebu fikiria mfano mdogo wako wa kiume aliyebarehe anaka mlangoni au kibarazani macho kayatumbulia kwenye kamba anaona kufuli(chupi)zako zilivuozagaa inakuwaje??.Kwa hiyo anjuwa kumbe Dada ana kufuli rangi hii,na ile na ile jamani.Sasa mfano ndo umeanika tu baba yako anaingia anakuta upepo umezidonsha kufuli mbichi kadhaa hapo chini.Atakuita we Fulani njoo nguo zimedondoka,au atainama aziokote na kuzitundika tena kambani ama???.Wengineo mpo kwenye nyumba za kupanga uswahilini huko Halafu unaanika mikufuli yako hovyo hovyo ndiyo nini??.Wadada wengi siku hizi wanahangaika na uzazi lakini ukiwachunguza kwa vipimo mahospitali unakuta wako vizuri lakini mimba hawapati na hawajui ni kwa nini.Moja ya sababu ni uanikaji hovyo wa nguo zao za ndani.Hapo umeanika mfano Mtu mbaya akaifanyia mazingara hujadhurika??.Ama watoto wakishaona hadharani hujiheshimu na minguo unaanika hovyo watakuheshimu kweli??.
Aaaah peleka huko.Wakati mwingine KUPIGWA MNAJITAKIA.
Joachim Mkwawa
mnyausiblog.blogspot.com

MUZIKI;WASAFI(WCB)WAANZISHA BENDI.

Lebo ya Muziki ya Wasafi chini ya CEO wake Diamond Platinums imeamua kukusanya wasanii mbalimbali na kuanzisha bendi.Uamuzi huo umekuja baada ya kuusoma vema mchezo na mwenendo ama muelekeo wa muziki ulivyo hivi sasa ndani na nje ya nchi.
Kundi hill La wasanii(bendi)linasemekana linaundwa na idadi kubwa ya wasanii waliyokuwa wakiunda kundi La Yamoto Band kipindi cha chuma.

Kwa mujibu wa chanzo chetu ni kwamba Wasanii kutoka Yamoto Band na ambao wanatarajiwa kuwa sehemu ya bendi hiyo mpya toka Wasafi(WCB)ni pamoja na Enock Bella,Mboso,Bella na wengineo buku msanii Lava Lava akitajwa kuwa kiongozi wa kundi hilo ndani ya bendi yao hiyo mpya.Huku msanii Aslay akikosekana ndani take.
Mnyausi News tutaendelea kukujuza hatua kwa hatua juu ya hili.

RELATIONSHIPS:-

THE REASONS WHY YOUR RELATIONSHIPS DON'T LAST.
Joachim Mkwawa.

Many Relationships these days take a drastic turn after few months.
Most time it's not intended,or planed by the partners but it becomes unavoidable so as to save the friendship that once existed.
These nosedive does not just happen it may be as a repetition of some characters or attitudes which one or both spouse detest.

Relationships are like newborns and must be handled as such else it will not survive.Your Relationships don't last because of these reasons listed below;

(1)You do not take each other into considerations before making vital decisions;
√As little as this may seem it has a way of making the other person feel insignificant or useless;the next thing on their mind will be how to exist the relationship.
It may even start building inferiority complex in them.Making them feel they are valueless and no one wants to stay where they are irrelevant.

(2)You did not take out time to check out your comparability;
√Many a times people jump into a relationship immediately they fell small butterflies in their stomach, not realizing that with time those will fly away as they came and they will be left with regality to face.
Whether we like it or not,the truth is we can not be comparable with everyone no matter how much we like them initially. True colors will start unfolding with time.

(3)You do not Realize that they have a mind of their own;
√Yes,most times we get blinded with love that we forget to remember that we are still dealing with Humans that have their sense intact and hence should have a mind of their own.So,most times when making decisions we should left them give their input, argue with ours and not.

(4)You are not open to change;
√Some of us have grown so rigid with time that we do not realize how important change is to is and the world of large.
When you a letting someone into your heart and space of large;You must take place with time because of individual differences. You should be ready to adjust some things to accommodate the other.
Relationships are all about little comprises from time to time.
By;
Joachim Mkwawa
Motivational Speaker
New Vision with Common Skills.
mnyausiblog.blogspot.com

If you find this to be true;please feel free to drop comments and share the article.

Jumatano, 18 Machi 2020

CORONA;WENGINE WAWILI WAGUNDULIKA NA KUTANGAZWA.

Nchini Tanzania ugonjwa wa Corona wawakumba watu wengine wawili;mmoja akiwa ni Raia wa Marekani aliyegundulika jijini Dar es Salaam na mgonjwa wa pili ni Raia wa Ujerumani ambapo yeye amegundulika akiwa visiwani Zanzibar.
Maambukizi hayo mapya yanafanya kufikia kwa idadi ya watu watatu ambao ndiyo waliyothibitishwa na kuripotiwa na Wizara ya Afya ya Tanzania kupitia Waziri wa wizara hiyo Mheshimiwa Ummi Mwalimu.

Wagonjwa hao watatu ni pamoja na yule mwanamama wa miaka 46 aliyeripotiwa juzi tarehe 16/03/2020 jijini Arusha ambaye ni Raia wa Tanzania akitokea nchini Ubelgiji.
Aidha Mheshimiwa Ummi Mwalimu amesisitiza kuwa Serikali imejiandaa vema kuhakikisha inapambana na Corona na kwamba kila mwananchi anapaswa kuchukua tahadhari kubwa kuhakikisha anajilinda dhidi ya maambukizi ya ugonjwa huu hatari.
Chanzo:Channel10

Jumatatu, 16 Machi 2020

CORONA YABISHA HODI TANZANIA.WAZIRI WA AFYA ATHIBITISHA.

Mapema asubuhi ya Leo Machi 16 Wizara ya Afya kupitia Waziri wake Mheshimiwa Ummi Mwalimu(MB)imesema kwamba mgonjwa hiyo ni mwanamke(46)Aligundulika kuwa na maambukizi ya virus 19 vya ugonjwa wa Corona.
Ikiwa hiki ndicho kisa cha kwanza cha ugonjwa huo kugundulika ambapo mwanamke huyo alisafiri akitokea nchini Ubelgiji kuja nchini Tanzania na kushuka Uwanja wa ndege wa Kilimanjaro(KIA).
Chanzo:Milad Ayo(Ayo TV)

Jumamosi, 14 Machi 2020

PRAYERS NEEDED HERE.

Joachim Mkwawa.

Please we're inviting you to pray with Gloria.
My name is Gloria;
I see how people pray for sick people on social media's. I have 3 kids and my husband is late.
Please pray for me as I want to do this surgery.I know some people will ignore me but remember you can be in my condition tomorrow.
I don't want to die;help me by praying and sharing this post to others.Am at the point of death.Please share it as much.

EDUCATION IS POWERFUL.

Education is more powerful in life.
That why we send our children to school to get education.
Education is tool which can be used for exploring the Universes and Lives of the Creatures.

Mnyausi News;
We're agreed that every child should go to school.
Yet in our Countries especially in our rural areas,Children are still burdened with early Marriage, engaged at farming and never feel even their Childhood time.
And those are exerctly the kind of reasons;That's make us Mnyausi News to start this campaign.
Every Child deserves a Childhood and it's up the rest of us to help remove the Barrie's that stand in their way.
"Please make it easier for all the masses".
Joachim Mkwawa
Motivational Speaker.

Ijumaa, 13 Machi 2020

IJUWE VIZURI CORONA NA JINSI YA KUJIKINGA NAYO.

Na Joachim Mkwawa.

Kila kona Duniani hivi sasa lugha inayoongewa ni moja tu.Nayo si nyingine ni juu ya kuenea kwa virusi vya ugonjwa wa ajabu na hatari wa Corona.
Corona unaripotiwa kuwa ni ugonjwa hatari sana ambao umekuwa tishio si tu kwa kukatisha uhai wa binadamu haraka Bali hata kudumaza ama kuwa tishio kwa uchumi wa Mataifa mbalimbali Duniani.Kwa Sasa kesi nyingi za Ugonjwa huu zinaripotiwa karibia Mabara yote Duniani na hasa kwa mataifa makubwa kama China,Italia,na kwingineko watu wakizidi kuambukizana na hata kupoteza maisha kwa wingi.
Basi kwa kuzingatia hayo Mnyausi News tumekuletea video yenye elimu juu ya ugonjwa huu hatari na namna ya kujikinga nao.

RAIS MAGUFULI ATOA TAHADHARI KUHUSU CORONA

Na Joachim Mkwawa.
Hii leo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.John Pombe Magufuli atoa onyo Kali kwa wananchi wake wote wa Tanzania juu ya ugonjwa hatari na tishio kwa uchumi wa Dunia;ugonjwa wa Corona.
Asisitiza kwamba Corona ni ugonjwa hatari na unaogharimu(kuua)maisha ya binadamu hataka kuliko magonjwa mengine.
Rais Magufuli akiongea hayo ameonya pia juu ya Tabia za watu wanaopenda kusafiri hovyo ndani na nje ya nchi.Kila Mtu katika familia yake nchini Tanzania anao wajibu wa kuchukua hatua kujilinda na kuelemisha wengine juu ya janga hili La Dunia.
Mtizame mheshimiwa Rais John Magufuli kupitia video hii.

ACHA MOYO WAKO UONGEE.

Habari za wakati huu ndugu mpendwa na msomaji wetu wa blog hii pendwa.
Nachukua fursa hii adhim kukueleza ya kwamba haijalishi ni yepi magumu unayapitia wakati kutokana na sababu mbalimbali za kimaisha.Naomba nikwambie kwamba yote unayoyapitia ni sehemu tu ya mchakato wa kukufanya ama kukutengeneza kuwa bora kulingana na hatima yako maishani.
USILIE.ACHA MOYO WAKO UONGEE.

Alhamisi, 12 Machi 2020

UTENGENEZAJI WA CREAM YA KUNYOLEA.

Na Joachim Mkwawa.
Yes,
Leo tena nakualika darasani mtafutaji mwenzangu,Mjasiriamali na mwanamaono mwenzangu uliye na uchu wa kuwa mzalishaji na mmiliki wa kiwanda ama biashara yako na kuwaajiri wengine.
Karibu tujifunze KUTENGENEZA CREAM YA KUNYOLEA.
CREAM hii ni maalum kwa ajili ya KUNYOLEA NYWELE sehemu mbalimbali za mwili bila kukusababishia vipele ama muwasho wa aina yoyote ile na inakuacha msafi,mkavu na mwenye amani hadi zitakapoota NYWELE zingine.Ndiyo...

MAHITAJI/MALIGHAFI:-
(1)Asali.
(2)Castile.
(3)Mafuta ya vitamin E.
(4)Majani mabichi ya Mlimao,Mchungwa,Mkaratusi na Lavenda.
(5)Maji.
(6)Bees Wax.

JINSI YA KUTENGENEZA.
(1)Pima Bees wax robo kg weka kwenye sufuria.
(2)Twanga majani mabichi ya Mchungwa,Mlimao,Mkaratusi halafu kamua Maji yake;na upime vijiko 3 vya chakula kisha tia kwenye sufuria yenye Bees wax.
(3)Pima Asali vijiko 2 tia kwenye hiyo sufuria.
(4)Chukua Castile kijiko 1 cha chakula tia kwenye sufuria.
(5)Tia mafuta ya vitamin E vijiko 2 vya chakula kwenye sufuria.
(6)Chukua Lavenda vijiko 2 vya chakula tia humo kwenye sufuria.
(7)Chukua Maji vijiko 3 pia vya chakula tia kwenye hiyo hiyo sufuria.
~Baada ya kuchanganya pamoja kisha tenga sufuria yako Motoni.Acha mchanganyiko uchemke kiasi huku umeufunikia.
~Kisha ipua mchanganyiko huo Acha upoe huku ukiwa umeufunikia.

Baada ya hapo ukiona tayari mchanganyiko umeshapoa;umimine kwenye tube(tyubu/vifungashio)uliyoiandaa ili kuihifadhi CREAM yako tayari kwa matumizi ya kupaka sehemu uliyonyoa au tayari kwa biashara.

MUHIMU:-
Hakikisha moto uwe mdogo sana pindi unaichemsha cream yako.

Hii ni cream mmoja nzuri sana na ukiipatia utauza sana maana inapendwa kuliko spirit.
KUMBUKA tu kwamba MALIGHAFI zote tajwa hapo juu zipo na zinapatikana tu kwenye maduka maalumu ya Wajasiriamali nchi nzima.Na kuhusu majani yanapatikana sana kwenye mazingira yetu ya kawaida majumbani.

Ahsante sana.
Ni Mimi;
Joachim Mkwawa
Email:joachimmkwawa8@gmail
Simu:+255 625887699
          +255 710590088

JE UNATAKA KUJUWA KUTENGENEZA SHAMPOO YA KUNG'ARISHA NYWELE?

Na Joachim Mkwawa.
Nichukue fursa hii kukukaribisha ewe mjasiriamali kwenye jukwaa hili pendwa kabisa La UJASIRI NI MALI(JIAJIRI).Mahala ambapo wajasiriamali na wazalishaji mbalimbali hujengwa na kuandaliwa kumiliki viwanda vyao binafsi vidogo vidogo.
Mada yetu Leo nataka UJUWE KUTENGENEZA SHAMPOO YA KUNG'ARISHIA NYWELE.
KUMBUKA:-
Hapa nakufunza kwa nadhalia lakini ukitaka kujifunza kwa vitendo Andaa muda wako na ada kidogo tu kisha nitafute ujifunze.Karibu darasani muda huu.

MALIGHAFI/MAHITAJI:-
(1)CDE
(2)Castile Soap
(3)Asali
(4)Distilled water
(5)Rangi
(6)Perfume.

JINSI YA KUTENGENEZA
(1)CDE nusu lita.
(2)Asali vijiko 3 vya chakula.
(3)Castile Soap robo kg.
(4)Distilled water robo lita.
(5)Rangi kijiko 1 cha chakula.
(6)Perfume vijiko 2 vya chakula.
(7)Changanya vitu vyote hivyo pamoja kama ulivyopima kwenye chombo kimoja.Koroga mchanganyiko huo kuelekea upande mmoja;hadi uhakikishe umechanganyika vizuri.

Na hadi hapo shampoo yako itakuwa tayari kwa matumizi.Ukitaka kuiuza basi nakushauri kwamba tafuta vifungashio tia humor shampoo yako,tia au bandika nembo yako tayari kwa biashara.Huhitaji kuweka chumvi.

Ahsante.
By
Joachim Mkwawa
Email:joachimmkwawa8@gmail.com
Simu:+255 625887699
          +255 710590088

JIFUNZE KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI.

Na Joachim Mkwawa.
Karibu tena ndugu msomaji na mjasiriamali mwenzangu katika dawati hili La UJASIRI NI MALI(JIAJIRI)ili uchote maarifa.
Na Leo nataka ujifunze KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI.

Sabuni hii ya MAJI unaweza itumia kudekia ndani kwako(nyumbani),kufulia au kama utataka kuitumia kwa ajili ya kusafishia maliwatoni(choo na bafu)Basi huna budi kuongeza kiwango cha perfume kidogo wakati wa kuitengeneza.
Hebu ungana nami hapa chini hatua kwa hatua ujuwe.

MAHITAJI/MALIGHAFI:-
(1)Salfoniki asidi nusu lita.
(2)Slees robo kg
(3)Sodash robo kg
(4)Maji lita 15
(5)Rangi nusu kijiko
(6)Sodiamu salfeti nusu kg
(7)Perfume vijiko 2
(8)Formaline vijiko 2
(9)Glyceline vijiko 4.

JINSI YA KUTENGENEZA.
(1)Andaa Diaba(jana)au chombo chochote cha ujazo wa lita 20.
(2)Weka Maji kiasi kwenye chombo chako.Hakikisha chombo chako ni kikubwa na kina ujazo unaozidi wingi wa Maji yako.
(3)Weka Salfoniki Asidi,Slees koroga kisha weka Maji tena na uendelee kukoroga kuelekea upande mmoja.Yaani unakoroga kuelekea kulia usigeuze kuelekea kushoto.
(4)Weka Sodash,Rangi uipendayo,Perfume, Formaline na Glyceline kisha endelea kukoroga mchanganyiko huo kwa dakika 2 au 3.
(5)Chukua chombo kingine cha plastiki mfano jagi au bakuli,chota huo mchanganyiko wako kiasi kupitia jagi au bakuli kisha chukua sodiamu tia kwenye hill jaki au bakuli lenye mchanganyiko uliyouchota toka kwenye jaba;halafu koroga ili sodiamu ichanganyike vizuri.Baada ya hapo mimina huo mchanganyiko wa kwenye bakuli au jagi umiminie kwenye ule mchanganyiko mwingi wa awali uliyomo kwenye jaba na uendelee tu kukoroga ndani ya jaba huku unaumimina mkorogo uliyomo kwenye bakuli au jagi.

Na hapo utaanza kuona mkorogo/mchanganyiko wako unaanza kupanda(kuongezeka/kuumuka)kuja juu.Kwa nini inakuwa hivyo??.
Ni kwa sababu Sodiamu huongeza wingi wa sabuni yako.Hivyo ukikoroga lita 15 hakikisha chombo chako kiwe kina ujazo wa lita 20 au zaidi.

Formaline husaidia kuitunza sabuni yako isiharibike haraka;yaani ukiweka Formaline basi sabuni yako inaweza kaa hata mwaka 1 bila kuharibika.
Ukimaliza,weka sabuni yako kwenye vifungashio(parkeg) tayari kwa biashara na matumizi.

KUMBUKA:-
Kuna aina 5 za Formaline.
(1)Formaline ya Chakula.
(2)Formaline ya Dawa.
(3)Formaline ya Sabuni.
(4)Formaline ya Maiti.
(5)Formaline ya kuzuia wadudu wasiharibu lotion.
Hivyo kuwa makini sana wakati wa kununua Formaline kulingana na uhitaji wako ama unakwenda kuitumia kufanyia nini.

MALIGHAFI zote hizo zipo na zinapatikana kwenye maduka maalum ya wajasiriamali nchi nzima.
Ukizingatia na kufuata vema hatua hizo hapo juu utakuwa hodari sana na mzalishaji mkubwa wa sabuni hii ya Maji.
Ahsante.
Wako ktk ujenzi wa Taifa
Joachim Mkwawa
Email:-joachimmkwawa8@gmail.com
Call/WhatsApp +255 625887699.

NAMNA YA KUTENGEBEZA SABUNI YA MCHE.

Na Joachim L.Mkwawa

Sabuni ya mche unawezaitumia kufulia,kuogea ama kuoshea vyombo nk.
Namna ya kutengeneza sabuni ya mche.

MALIGHAFI:-
(1)Mafuta ya Mbosa/mawese/Nazi Lita 4.
(2)Maji mililita 350×4=1400;ambazo ni sawa chupa 4 za soda zilizojaa vizuri.
(3)Caustic Soda 0.5kg
(4)Sodash 0.5 kikombe cha chai.
(5)Perfume.
(6)Box.

JINSI YA KUTENGENEZA:
Zingatia hatua zifuatazo pamoja na vipimo kama ninavyoelekeza ili utengeneze kitu bora,salama na chenye uhakika sokoni.
(1)Loweka Caustic Soda 0.5kg kwenye maji mililita 1400.
~Koroga na uifunike.Uache mkorogo huo ulale Massa 24 had I kesho.
(2)Kesho yake pasha moto mafuta.
~Ipua acha yapoe ibakie joto kiasi.
~Kisha yamimine mafuta hayo kwenye chombo kingine cha plastiki.
(3)Chukua Caustic Soda uliyoikoroga jana imimine kidogo kidogo kwenye chombo kile cha plastiki ulichoweka mafuta; huku ukikoroga haraka haraka kuelekea upande mmoja.
(4)Baada ya hapo koroga Sodash kwenye chombo kingine,kisha imimine kwenye mchanganyiko wa Caustic Soda na Mafuta huku ukiendelea kukoroga kuelekea upande mmoja.
(5)Weka perfume vijiko 2 vya chakula kisha koroga hadi uji uji use raini kabisa.
(6)Andaa box;mimina mkorogo huo ndani ya box.Acha ilale humor hadi kesho yake.
(7)Baada ya hapo utakata vipande vipande uvitakavyo wewe na Sabuni yako ya mche itakuwa tayari kwa matumizi.

Kwa maelezo zaidi ama kujifunza kwa vitendo tafadhali wasiliana nami kupitia +255 625887699 au +255 710590088.

Jumatano, 26 Februari 2020

FUNGUO 10 ZA HEKIMA NA MAFANIKIO.

Na Joachim Mkwawa.
Katika maisha ya kila Siku ya mwanadamu kitu mafanikio ni jambo muhimu sana kwake.Lakini vipi na kwa namna gani atafanikiwa ndivyo vitu ambavyo hufanya wengi washindwe kufanikiwa.
Leo nimekuletea
FUNGUO 10 ZA HEKIMA NA MAFANIKIO.
(1)MIPANGO
>Mafanikio yako hutegemea sana ubora wa mipango yako ya maandalizi.
>Moja ya sababu za kutokufanikiwa no kutokuwa tayari kutenga muda kwa ajili ya kupanga malengo thabiti.
>Mipango huleta kujiamini,kujali,kuheshimi na kukupa Ari ya kuitimiliza.
>Kitu cha muhimu katika ndoto zako ni kuwa na Mpango makini pamoja na Mpango kazi unaotekelezeka.
>Mipango huondoa migongano isiyo ya lazima.

(2)UTULIVU WA AKILI.
>Mbegu ya Mafanikio huota,hukua na kumea vema palipo na Amani.
>Usifanye chochote kinachousumbua moyo na kuitesa roho na nafsi yako.
>Gundua kile kinachokutia hamasa na kuamsha hisia na fikra zako katika maisha ili kufanikiwa.
>Mile kinachokupa Amani moyoni ndicho muhimu sana hasa kwa maisha yako.
>Chochote kiletacho furaha,Amani na nguvu ndani yako;ni alama ya kile Mungu anachotaka ufanye.
>Fanya kile unachokiamini na kukipenda kwani ndicho hukutafsiri.
>Itii dhamiri yako,ni ufunguo wako wa Mafanikio.

(3)NDOTO YAKO,MLENGO WAKO.
>Ndoto yako huhitaji sana mlengo wako wote.
>Mlengo wako utakufanya use MTU wa shauku,mbunifu na mvumilivu.
>Maisha ni safari hivyo yakupasa uwe na muelekeo.
>Ndoto yako huanzisha na kuchochea nia iliyo moyoni mwako.
>Mambo makubwa kwa kawaida huanza na mambo madogo.Mti mkubwa huanza na mbegu Ndogo.
>Watu Kushindwa kufanikiwa kwa sababu ya kuwa na muelekeo mbovu.
>Maisha yako ya kesho(baadaye)huanza na kile ulichonacho Leo mkononi mwako.

(4)MAUMIVU/MACHUNGU
>Kila aliyefanikiwa aligundua kuwa maumivu ni ya muda.Yatapita,ni njia ya kuelekea Mafanikio.
>Mtu hazami kwa kuangukia tu kwenye maji,Bali huzama endapo ataendelea tu kubaki ndani ya maji.
>Usiharibu ndoto,mipango,malengo na maisha yako ya baadaye kwa kufikiria tu maumivu yako ya nyuma.
>Huwezi zuia misiba isitokee,Bali unaweza kuikwepa isikuharibu wewe.
>Watu wakuu wamepitia maumivu makubwa.Mateso yako ni njia ya kuelekea miujiza yako mikubwa.
Jifunze kuvumilia na kuwa tayari kuzikabili changamoto ili kuifikia hatima yako maishani.

(5)UPENDELEO
>Usidharau wema unaotendewa na Watu.Siyo kitu kidogo katika Dunia hii kubwa.Ni kitu kikubwa sana katika Dunia hii ndogo.
>Wape wengine nafasi ya kwanza ili kupanda mbegu ya kupendelewa na kufanikiwa ama kufanikishwa katika maisha.

(6)HARAKA HARAKA
>Ndoto kubwa huhitaji muda zaidi.
>Unapoharakisha;Unaongeza makosa katika mambo yako.
>Fanya mambo kwa usahihi tokea mwanzo.
>Tumia vena muda wako ili kufanya mambo yako kwa usahihi.
>Mafanikio katika maisha hayaji kama ajali.
>Mafanikio ya maisha humgharimu MTU.
Hivyo lazima utambuwe kuwa itakugharimu wewe kufikia ukuu.Itakugharimu muda,nguvu,msimamo,kujitoa,kujituma,kujinyima na kuvumilia.

(7)MUDA
>Anayetumia muda wake vizuri hutawala maisha yake.
>Usipoteze muda.Ni mfupi sana,wenye thamani na haupatikani tena.
>Usiiache Siku ipite hivi hivi tu.
>Epuka kupoteza muda wako na marafiki,maongezi yasiyo na tija wala manufaa kwako.
>Watu wakuu huzitumia siku zao vizuri.
>Wasiyoheshimu muda wako,hawata heshimu HEKIMA yako.
>Muda ni pesa.

(8)KUSHINDWA
>Kushindwa hakuwezi kukutokea pasipo ruhusa yako.
>Kila binadamu hufanya makosa.
>Ushindi huenda kwa yule asiyekata tamaa.
>Kila Mtu hushindwa.Lakini wanaoshindwa huanza upya baada ya Kushindwa.
>Washindi huwa hawakubali Kushindwa.
>Vita ni vya wale waliyo wavumilivu.
>Maisha siyo mwendelezo wa Kushindwa;Bali huwa ni gwaride La miujiza.
>Acha kushughulikia mambo ya Jana.
>Mungu huwa haangalii yaliyopita ili kuamua hatima ya maisha yako ya baadaye.
>Kushindwa kwako huandaliwa na kuzimu Lakini Mafanikio yako huandaliwa na Mbingu.

(9)URAFIKI NA USHIRIKIANO
>Wasiyokuongezea kitu,Hukupunguzia kitu.
>Siyo Kila wanachokiongea Watu juu yako ndiyo muhimu.Ila kile unachokiamini wewe juu yako ndiyo muhimu.
>Washindi huwa hawafanikiwi peke yao.Bali hukishinda kiburi chao.Hukataa kuwa wapweke.
>Kila Mtu ni kisima cha taarifa.Chota kutoka kwake.
>Unachowafanyia Watu; Mungu hufanya kitokee kwako pia.
>Sifa zako nzuri zitaonekana mbele ya watu wazuri.
>Lipa gharama ili ukae miongoni mwa watu wa kawaida ili ufanikiwe.
>Usiongee matatizo yako na MTU ambaye hataweza kukusaidia kuyatatua.
>Marafiki hutofautiana;chagua wale wanaokuchangamsha,wanaokuelimisha na kukupa faraja.
>Hatua ya kwanza kuelekea kwenye Mafanikio ni kuwa tayari kusikiliza.
>Tumia HEKIMA ya watu wakuu ili ufanikiwe.
>Tumia vizuri nguvu au Mafanikio ya wengine.
>Mwongozo au ustawi ni ufunguo wa kufanikiwa.

(10)MABADILIKO
>Huwezi kuyabadilisha maisha yako hadi ubadili Yale uliyozoea kuyafanya kila Siku.
>Wakati mwingine hukulazimu ufanye kile usichokipenda ili upate kile unachohitaji na kukithamini.
>Huwezi kuinuliwa hadi utoke kwenye nafasi uliyopo sasa.
>Huwezi kusahihisha kile ambacho hauko tayari kuchukua hatua ya kukabiliana nacho.
>Hali ya maisha yako hutegemea sana mtazamo wako.
>Huwezi kufika unakokuhitaji kama hujaamua kunyanyua mguu  kutoka hapo ulipo na kupiga hatua kwenda kule unakokutaka uwe.
>Huwezi kufikia malengo yako mpaka uyape kipaumbele katika mambo yako.
>Matatizo hutokea pale panapotokea mabadiliko.
>Kadiri unavyoendelea kukaa na tatizo ndivyo utakavyoshindwa kupata ufumbuzi.
>Leo ni kesho inayoongea kuhusu Jana.

JINSI YA KUKUZA BIASHARA YAKO.

Newvisionskills.com

Fubguo za hekima na Mafanikio.

(1)Mipango.

(2)Utulivu wa akili.

(3)Ndoto yako,Mlengo wako.

(4)Maumivu/Machungu.

(5)Upendeleo.

(6)Haraka haraka.

(7)Muda.

(8)Kushindwa.

(9)Urafiki na Ushirikiano.

(10)Mabadiliko.

Jumanne, 25 Februari 2020

UJASIRI NI MALI(JIAJIRI)

JINSI YA KUKUZA BIASHARA YAKO.
(1)Ongeza idadi ya wateja(Increase the Number of Customers)
Ongeza idadi ya wateja wako kwa kujitangaza.Fanya matangazo kuwafikia watu wengi na kuweza kuongeza wateja kwenye biashara yako.

(2)Ongeza idadi ya mauzo/manunuzi ya kila mteja(Increase the Unit of Sales)
Ikiwa kila mteja anakuingizia wastani wa shilingi elfu 10 tu kwa kila manunuzi yake;inakulazimu ujitahidi kumshawishi mteja huyo anunue na bidhaa zingine za ziada ambazo zitakufanya uongeze mapato yako kwa kila manunuzi yake kwako.
Mfano:-
KFC na McDonald hasa ni hodari sana katika hilo.Kwao ukiweka oda ya burger;watakuuliza ,"He,utapenda tukuwekee na chipsi?".Ukisema ndiyo pia watakuuliza tena,"Utapenda tukuwekee na kinywaji gani?".

Hivyo hapo utakuta lengo la mteja nilikuwa anunue burger lakini watajikuta wameuza chipsi na kinywaji zaidi kwa mteja wao.

(4)Ongeza Unafuu,Ubora na Uhakika wa bidhaa ama huduma yako.
Ujitahidi sana kuwa tofauti na wengine kwa kuongeza Unafuu wa gharama kwenye bidhaa ama huduma yako.Pia hakikisha unakuwa na bidhaa au huduma bora na zenye Uhakika wa upatikanaji wake kila zinapohitajika.
Mfano:-
Kuwa na mawasiliano mazuri na wale wanaokuuzia mzigo wa jumla ili kujuwa ingizo jipya la mzigo mpya ili uwe wa kwanza kupata bidhaa hizo kabla ya wengine unao chuana nao kibiashara.

(5)Uwe muaminifu.
Jenga uaminifu kwa wateja wako.Jenga uaminifu kwa jamii yako na lakini pia kuwa muaminifu kwa kipato kitokanacho na biashara yako.Kuwa muaminifu hata kwa wale wanaokusaidia kazi na majukumu mengine kwenye biashara yako.