Na Joachim Mkwawa
Motivational Speaker.
Habari mwanadawati mwenzangu wa dawati hill la UJASIRI NI MALI(JIAJIRI).
Dawati ambalo kimsingi hukujenga na kukuhamasisha katika kujiajiri wewe mwenyewe ama kuwekeza hata kama upo katika ajira rasmi.
Dawati hill kipekee ndilo hupatikana na kutukutanisha wajasiriamali kupitia blog hii pendwa Duniani kote.Na Leo nimewiwa kukushirikisha hatua ama mambo muhimu ya kuzingatia ikiwa unataka KUBAKI KUWA MASIKINI MAISHANI MWAKO.
JINSI YA KUBAKI KUWA MASIKINI.
Yamkini unaweza usinielewe;lakini kufuatia hatua hizi naamini ukizifuata na kuzifanyia kazi kikamilifu hakika lazima ubaki kwenye umasiki.
(1)Kamwe usiamke mapema,Endelea kulala na kujinyoosha.We lala tu hadi jua litakapochomoza,yaan hakikisha unalala hadi uone mwanga wa ndani kwako unafana na wa nje.Au lala hadi njaa itakapokuuma ndipo uamke.
(2)Kamwe usipange namna sahihi ya kuitumia pesa yako.We zitumie tu utakavyo hasa pale unapozipata.Na zikiisha hata usipoteze muda kukaa chini na kufikiria ulizitumiaje.
(3)Kamwe usiwaze wala kufikiria ku-save pesa yako,subiri hadi upate pesa nyingi ndipo uanze ku-save.Uta-save vipi pesa yako wakati unazo kidogo!??.Tena wapuuze wale wote wanaokushauri ku-save kwani hawakutakii mema wewe na pesa yako.Watakupangiaje kutumia pesa yako ilihali hawakukusaidia kuitafuta??.
(4)Kamwe usijiingize kwenye biashara ambazo huwa mnaziita za kitoto tena ni za watu wasiyosoma.Wewe ni msomi bwana na tena umemaliza chuo kikuu,umeajiriwa na halafu unalipwa vizuri mshahara mkubwa.Sasa ya nini ufanye biashara za kuuza Viazi?,Utauzaje mbogamboga?,Yaani na usomi wako halafu ukauze viatu vya mtumba kweli?.We msomi bwana hupaswi kufanyaje biashara za watu wasiyosoma aisee.Wewe unafaa ukae tu ofisini upigwe na kiyoyozi Basi.Una shida gani kwani.
(5)Kamwe usifikirie kuanzisha biashara mpaka pale Malaika atakaposhuka kutoka Mbinguni akuletee mtaji mkubwa wa kuanzisha biashara.Kwa wakwambie uanzishe biashara hata kwa mtaji mdogo eti kisa wafanyabiashara wengine wakubwa kama akina MO au Bakhresa walianza kwa kuuza migahawa.Wewe ni smart bwana unatakiwa uanze na mamilioni.Sawa eeeh!??.
(6)We lalamika kuhusu kila kitu Ila Kamwe usilalamike kuhusu uvivu wako na Attitude yako.We ilaumu tu Serikali ya Magufuli kwamba imekaza vyuma,Lalamikia benki zisizotaka kukuamini na kukukopesha mtaji,laumu makampuni mbalimbali yaliyokunyima ajira ama yaliyokufuta kazi.Kwa sababu wote hao ni wabaya na hawataki wewe uwe tajiri.
(7)Tumia pesa nyingi kuliko kipato chako.Na ili kufanikisha hilo wewe tununua bidhaa kwa mkopo,azima pesa kwa rafiki zako,nunua samani nzuri za ndani,Nunua Brand New LG flat screen.Kopa pesa benki ama kazini kisha kanunue gari Kali na ya kisasa ya kutembelea.Honga vyovyote vile utakavyo hadi mjini wakukome.Ndiyo pesa si ni zako bwana;unakwama wapi?.
(8)Shindana katika kuvaa.Hakikisha hupitwi na fashion yoyote mpya ya nguo,viatu,gari na simu.Nunua kila aina ya simu inayotoka yaani usikubali kupitwa na Toledo jipya la simu;hata kama ulikuwa na Samsung Galaxy S6 uliyoinunua milioni 1 we iuze tu hata kwa laki 7 kisha ongezea pesa kiasi uende kununua Samsung Galaxy S7.Ndiyo kwa sababu hizo simu kalikali zimetengenezwa kwa ajili yako bwana.
(9)Ukishindwa kununua gari mpya,Nunua hata used lakini Kali na ambayo gharama zake kwenye kuihudumia ni mara 2 ya mshahara wako ama inayodumu muda mrefu.
(10)Halafu mwisho sawa wala usiogope maneno ya watu.Maana watu kama wewe msiyokuwa serious na maisha huwa hamzeeki wala nini.Endelea kuishi hivyo hivyo.
Fainali ni uzeeni.
Hivyo ajili za kuambiwa vema ukachanganya na za kwako.
Ukifanya kinyume na hizo hatua lazima utatajirika na ikiwa utazifuata na kuzitii vema hizo hatua Basi naamini umasikini utakuhusu.
Mimi ni
Joachim Leonard Mkwawa
Motivational Speaker
mnyausiblog.blogspot.com