Jumatatu, 31 Desemba 2018

KUPIGWA TUNAJITAKIA

Ni kweli kabisa.
Kupigwa huwa hakuji tu hivi bila sababu ingawa kujichukulia nako sheria mkononi na kumuadhibu mtu kisa amekukwaza ama vyovyote vile huwa ni kosa kisheria.

Lakini hapa binafsi najikita katika ile hali mkosaji kuamua kutenda kosa ilihali anajuwa fika kwamba kutenda jambo hilo ama lile kwa makusudi ni makosa

Je,kwa makosa haya kweli unadhani huyu mtu akiadhibiwa ni makosa?
Huyu a

HERI YA MWAKA MPYA 2019.

Uongozi pamoja na wote wanaohusika kwa namna moja au nyingine katika kuhakikisha blog hii inakufikia na kukuhabari,kukuelimisha na kukubirudisha tunakutakia heri ya Mwaka mpya 2019.

Tunatanguliza shukurani zetu za dhati kwenu wote wasomaji na wafuatiliaji wa blog hii.
Tunaomba radhi kwa usumbufu uliyojitokeza kutokana kulikuwa na nyakati ambapo blog hii hakuweza kurusha matangazo yake,lkn bado mliendelea kutuamini na hivyo mkatuvumilia.

Mwaka 2018 tunashukuru umepita salama ingawa kwetu ilikuwa na changamoto nyingi sana ingawa tumezishinda na ndiyo maana leo tuko hapa tena tukiwashukuru.

Mwaka 2019 ni mwaka wa Mageuzi makubwa kwetu kitaaluma,kiufundi na kiteknolojia na hivyo tumejiandaa sana kuwahudumia.
Palipo na mapungufu sisi km binadu tunaomba mtusamehe.
Heri ya Mwaka mpya 2019.

WAARABU WA KUIZIMA SIMBA SC KLABU BINGWA AFRIKA.

Mabingwa wa Ligi kuu Bara nchini Tanzania timu ya Simba Sports Club ya jijini Dar es Saalam wiki iliyopita imefanikiwa kutinga hatua ya Makundi ktk michuano ya Kimataifa ya kuwania ubingwa wa Afrika kwa ngazi ya vilabu.

Simba SC imefikia hatua hiyo baada ya kuiondosha mashindanoni timu ya Nkana FC ya nchini Zambia majuma mawili yaliyopita katika mchezo wa marudiano uliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Daalam...,kwa kuichapa Nkana jumla ya bao 4 kwa 3,ikiwa ni bao 2-1 Waliyoshinda Nkana kule Zambia na 3-1 waliyoshinda Simba jijini Dar es Salaam.

Matokeo haya yakaipa Simba kibali cha kutinga hatua ya makundi ambapo Ijumaa ya juzi baada ya droo ya makundi kuchezeshwa timu hiyo ya Simba ikajikuta imo kundi D ikiwa ni moja kati ya timu 4 zinazounda kundi hilo.
Katika kundi hilo kuna timu 2 za Uarabuni ambazo ni Al Ahly ya Misri na JS Soura ya Algeria huku timu zingine 2 katika kukamilisha timu 4 katika kundi D zikiwa ni AS Vita pamoja na Simba yenyewe.

Kwa mara kadhaa wababe wa Soka nchini Tanzania klabu za Simba,Yanga na Azamu wamekuwa wakishindwa kutamba mbele ya timu zitokazo falme za Kiaarabu na hasa katika michezo mbalimbali pindi timu hizo zikicheza katika viwanja vya nchi mwao(Uarabuni)

Viongozi,Wanachama,Wachezaji na Mashabiki wa timu hiyo ya Wekundu wa Msimbazi yenye maskani yake mtaa wa Msimbazi Kariakoo jijini Dar es Saalam wanasisituza kwamba mwaka wao huu hivyo wanawaonesha Waarabu kabumbu la aina yake na hasa ukizingatia wana kikosi kipana na chenye uwezo wa kushinda mahali popote.

  Timu ya Simba inaundwa na wacheza wengu,nguli na wenye majina makubwa Afrika Mashariki na kati kamq vile M.Kagere,E.Okwi,C.Chama,S.Kichuya,P.Wawa,A.Manula,S.Kapombe,Mo,Dilunga,Kotei,Boko na wengine wengi.

Hata hivyo timu ya Simba bado ina kibarua kingine cha kuhakikisha walau inatinga robo fainali katika michuano hiyo ili kujihakikishia kucheza tena hapo mwakani kwani hivi juzi imeondolewa katika ligi ya kombe la shirikisho na timu ya daraja la kwanza iitwayo Mashujaa toka pale mkoani Kigoma.
Tunasema hayo kwa sababu hata katika ligi kuu Bara hapa nyumbani mahasimu wao wakubwa timu ya Yanga wanaonekana kuupania vema ubingwa wa mwaka huu kwani hadi sasa wameshajikusanyia pointi 50 kibindoni katika jumla ya michezo 18 waliyocheza  bila kupoteza hata mmoja huku wakishinda michezo 16 na kutoka sare 2 na kufanya waongoze ligi huku wakiwa wamebakiwa na mvhezo 1 ili wafunge mzunguko wa kwanza mbele ya Azam wenye point 40 kwa michezo 17 waliyocheza huku Simba wakiwa nyuma na pointi zao 33 walizokusanya katika michezo14 waliyocheza na wakiwa na kiporo cha mechi 6 mkono kukamilisha mzunguko wao wa kwanza katika ligi kuu Bara.

Mungu ibariki Simba Sports Club
Mungu ibariki Tanzania.
Kila lakh

Jumapili, 21 Oktoba 2018

CHEKELEA UONGEZE SIKU ZA KUISHI.

Uswahilini kuna vituko.
Vunja mbavu kidijitali.

SIMBA WAMPA POLE MO DEWJI KWA KUICHARAZA STAND UNITED 3-0

Hii leo kunako dimba la Taifa kumeshuhudiwa mchezo wa nguvu ukiwakutanisha mabingwa watetezi Simba SC ya jijini Dar es Saalam dhidi ya Stand United ya Shinyanga.
Ambapo hadi dakika 90 za mchezo kumalizika Simba ilitoka kifua mbele kwa ushindi mnono wa magoli 3 kwa 0 huku magoli hayo yakitiwa kimiani na wachezaji  Cletous Fhama mnamo dakika ya 30 wakati la pili likifungwa na Emmanuel Anord Okwi huku lile la 3 likiwa ni la kujifunga Stand Utd wenyewe baada ya kutokea harakati za uokoaji wa mpira wa kona ulipigwa na Shiza Ramadhan Kichuya mnamo dakika ya 86 ya mchezo.

Kwa ushindi huo ni kudhihirisha kwamba kile walixhokieleza wachezaji kabla mchezo huu hapo jana ni kwamba watashinda mechi hiyo ya kesho(leo)ili iwe ndiyo pole yao kwa Boss wao aliyekuwa kapotea kwa kutekwa kwa zaidi ya siku 8 kabla ya kupatikana usiku wa kuamkia jana.

Mbali na hivyo Simba watakuwa wameendelea kujiweka pazuri zaidi ktk msimamo wa ligi kuu Bara wakiwa na pointi zao 17 kwa michezo 8 nyuma ya mahasimu wao Yanga SC wanye pointi 19 kwa michezo 7 huku vinara ktk msimamo huo wakiwa ni Azam FC zote za jijini Dar es Saalam.

Jumamosi, 20 Oktoba 2018

Yanga yaiua Alliance Sports Club goli 3 kwa sifuri hii leo uwanja wa Taifa jijini Dar es Saalam.

Mchezo huo uliyokuwa wa vuta nikuvute ikishuhudiwa vijana wa Alliance kujaribu mara kadhaa kuliandama lango la Yanga,lakini hata hivyo juhudi hizo hazikuzaa matunda ambapo mnamo dakika ya 17 ya mchezo H.Makambo aliiipatia Yanga goli la kwanza,huku winga machachali Mrisho Khaphan Ngasa akifunga goli la pili mnamo dakika ya 29 ya mchezo kabla ya mapumziko.Na baadaye kipindi chapili Ibrahim Ajibu Migomba akamaliza kazi kwa kuipatia Yanga goli la 3 dakika ya 86 ya mchezo.

Hadi dakika 90 za mchezo Yanga 3 na Alliance 0

Ijumaa, 19 Oktoba 2018

CHADEMA BADO NI HAI.

HIZI HAPA SERA ZAO KAMA CHAMA:
Chama cha Demokrasia na Maendeleo nchini Chadema bado kimeendelea kijijenga kama chama mbali ya kashikashi zinazopitia kama chama ikiwemo hamahama za baadhi ya waliokuwa Madiwani na wabunge kupitia chama hicho kuamua kijivua nyazifa zao na kukihama chama na kukimbilia chama tawala kwa sababu zao mbalimbali na kubwa hasa ikiwa ni kule kuunga mkono juhudi za serikali iliyopo madarakani inayoongizwa na chama tawala CCM.

Mbali na hayo pia chadema ilipoteza majimbo na kata mbalmbal katika chaguzi za marudio huku chama tawala CCM ikijishindia bafasi hizo huku ikiwatumia viongozi haohao waliyoikimbia Chadema ili kuiwakilisha CCM katika chaguzi hizo.

Chadema kuonesha ni jasiri,wakomavu na wenye nia thabiti kuelekea chaguzi za Serikali za mitaa 2019 na ule uchaguzi mkuu 2020 wameendelea kujijenga na kuanza kuweka wazi sera zao.
Jionee hapa chini.

MANJI RASMI YANGA.

WANACHAMA NA MASHABIKI MENO NJE NJE.
Habari ndiyo hiyo unaambiwa.
Ni kwamba Mara baada ya kujiweka pembeni dhidi ya soka na hasa timu ya Yanga kwa zaidi ya siku 517 ambazo ni sawa na mwaka 1 na miezi 4 na siku 29...,hatimaye Tajiri,mfadhiri,mwenyekiti na kipenzi cha wana Yanga Bw.Yusuph Manji amerejea na kutambuliwa kama ndiye mwenyekiti wa klabu hiyo kongwe na mabingwa wa kihistoria kunako tasnia ya kandanda nchini Tanzania.

Yusuph Manji alitangaza kujiuzuru kuitumikia Yanga km Mwwnyekiti mnamo mwezi Mey tarehe 20 mwaka 2018.
Kutokuwepo ama kutojihusisha kwake dhidi ya Yanga kuliifanya timu hiyo kuyumba kiasi fulani kiuchumi,kiufundi na hata kushindwa kuutetea ubingwa wao waliyokuwa wakiushikilia kwa matatu mfurulizo hadi mwaka jana.
Mbali hayo timu ilishindwa hata kusafirisha wachezaji baadhi ilipitakiwa kucheza ugenini(mikoani) mfano wa ile mechi kati yao na timu mojawapo ya jijini Mbeya mwaka jana.

Hayo,ni matikeo ya kikao cha kamati ya uchaguzi ndani ya klabu hiyo kilichokaaliwa juzi jumatano  ambapo kilitoka na maazimio ya kumrejesha na kumtambua Manji kama ndiye Mwenyikiti wa timu hiyo huku kamati hiyo ikisisitiza kwamba nafasi zilizowazi na zinazotakiwa kupata viongozi ni Makamu mwenyekiti pamoja nafasi za wajumbe ambao waliyokuwepo awali walijihuzuru nyazifa zao wakiwemo;Salum Mkemi,Hashim Abdallah na Omar Saidi kutoka Tanzania Visiwani(Zanzibar),Huku Ayoub Nyenzi kwa kutohudhuria vikao mfururizo vya kamati hiyo hivyo naye alipoteza sifa za kuwa mjumbe wa kamati hiyo ya Utendaji ndani ya klabu.

Itakumbukwa pia nafasi ya makamu mwenyekiti ilikuwa chini ya Clement Sanga aliyejihuzuru nafasi hiyo.

Hata hivyo Katibu mkuu wa klabu hiyo Bw.Omary Kaya alieleza kwamba habari zote kuhusu Mwenyekiti alidai lipo chini ya kamati ya uchaguzi ambayo ndiyo yenye dhamana ya kulisemea hilo huku  mjumbe wa kamati ya uchaguzi wa Yanga,Bakili Makele alisema kuwa ufafanuzi wa zoezi la uchaguzi na kwamba ni lini utafanyika na habari zote za Manji utatolewa kwenye mkutano na vyombo vya habari muda wowote kuanzia leo Ijumaa.

Wakati hayo yakielezwa na viongozi hao huku wadau,wanachama na mashabiki kindakindaki wa timu hiyo kongwe nchini wameonekana wakifurahia urejeo huo wa bosi huyo kipenzi wa Yanga huku wakitamba kwamba taji la ubingwa ni lao na kwamba wao ndiyo wanastahili kukwea pipa(kupanda ndege)kwenda kuiwakilisha nchi ktk medani za kimataifa.

JIAJIRI MWENYEWE.

UJASIRI NI MALI.
Kwa mahitaji yako yote ya VIATU vya Kimaasai kwa Jumla na rejareja karibu NEW VISION with COMMON SKILLS,DODOMA TZ.

Kwetu utajipatia viatu aina zifuatazo.
(1)Viatu vya kike vya ngozi
(2)Viatu vya kike vya ngozi yenye manyoya.
(3)Viatu vya Kike vya kitambaa
(4)Viatu vya kike vya shanga.
(5)Viatu vya kiume vya ngozi
(6)Viatu vya kike vya shwapa.
Tupigie +255625887699
Whatsapp:+255629108340
Instagram:joachimmkwawa

Jumatano, 17 Oktoba 2018

UJASIRI NI MALI.

JIFUNZE KUTENGENEZA SABUNI YA KUFULIA YA MAJI.

Leo tena bado tupo hapa kukuhamasisha na kukufunza namna ya kujiajiri wewe mwenyewe.Jifunze tena Fursa hii adhimu.

Sabuni hii ya maji unawezaitumia kwa kudekia sakafu yako,kufulia ama kuoshea vyombo vyako nyumbani.

(1)MAANDALIZI.
(a)Beseni kubwa au Diaba.
(b)kijiko.
(c)Mwiko.

(2)MAHITAJI/MALIGHAFI.
(a)Salphonic acid nusu Lita.
(b)Sless robo Lita
(c)Sodash robo kilo.
(d)Maji Lita 15.
(e)Rangi nusu kijiko.
(f)Sodium salfet nusu kilo
(g)Perfume vijiko 2.
(h)Formaline vijiko 2
(j)Glyceline vijiko 4.

(3)JINSI YA KUTENGENEZA.
(a)Andaa Diaba(jaba)au chombo chochote mfano beseni lenye ujazo wa Lita 20.
(b)Weka maji kwenye chombo hicho na hakikisha chombo chako ni kikubwa kuzidi wingi wa maji yako.
(c)Weka sulphonic acid,sless vyote kama ulivyoelekezwa na kuvipima kwa vipimo tajwa hapo juu.Vichanganye kupata mkorogo ama mchanganyiko mmoja bila kuukoroga lakini ukiwa undani ya jaba lako.
Tia maji yote Lita 15 kwenye jaba na uanze kukoroga kuelekea upande mmoja yaani kama unakoroga kuelekea kulia usigeuze kuelekea kushoto.
(d)Weka sodash,Rangi uipendayo iwe bluewax,greenwax ama redwax.Tia perfume,Formaline na Glyceline kisha endelea kukoroga mchanganyiko huo kwa dakika 2 au 3.
(e)Chukua chombo kingine cha plastic mfano jagi au bakuli kisha chota huo mchanganyiko wako kiasi halafu utie sodium kwenye bakuli au jagi hilo na ukoroge vizuri.

(f)Kisha mimina mkorogo huo wa kwenye bakuli au jagi kwenye ule mchanganyiko wako wa awali uliyopo kwenye jaba na endelea kukoroga na hapo utaona mchanganyiko unaanza kupanda juu.Hii ina maana kwamba Sodium huingeza wingi wa sabuni yako.

Hivyo ukikoroga Lita 15 hakikisha chombo chako kina ujazo wa Lita 20 au zaidi.
Na Formaline husaidia kuitunza sabuni yako isiharibike haraka yaani ukiweka formaline basi sabuni yako yaweza kaa hata mwaka 1 bila kuharibika.

Baada ya hapo  yaani umemaliza kutengeneza chukua sabuni yako na mimina katika vifungashio ulivyokwisha kuviaandaa,weka lebo yako.Na tayari sabuni yako itakuwa tayari kwa matumizi ama biashara.

Na hii itakuwa ni sabuni safi,nzuri,yenye kunukia,raini isiyochubua mikono ama kufubaza nguo na itakayokuoa matikeo mazuri kwako na sikoni.

Kumbuka.
Zipo aina 5 za Formaline hivyo kuwa makini pindi unapokwenda kununua malighafi zako dukani.Na malighafi hizi hupatikana kwenye maduka maalum ya ujasiriamali tu na vinginevyo.

Aina za Formaline
(1)Formaline ya chakula
(2)Formaline ya kutunzia dawa
(3)Formaline ya kutunzia sabuni
(4)Formaline ya kutunzia maiti
(5)Formaline ya kuzuia wadudu wasiharibu lotion(losheni).

Ahsante sana naomba niishie hapa kwa Leo.
Kesho tena usisite kutufuatilia ili kujuwa tumekuletea kitu gani cha kujifunza kutengeneza na kukufanya ukajiajiri wewe mwenyewe ukajiingizia kipato..

Piga +255625887699

UJASIRI NI MALI:-

JIFUNZE KUTENGENEZA SABUNI YA KUFULIA YA UNGA.
Ktk ulimwengu wa leo kila kukicha bado mahitaji ya kibinadamu yanazidi kuongezeka.Mahitaji hayo mengi yapo ktk umuhimu mkubwa wa binadamu kutaishi mazingira.

Maisha ya binadamu yanategemeana kati ya binadamu mmoja dhidi ya mwingine.Yaan ili mwanadamu Fulani apate anachohitaji ni lazima ampe binadamu mwenzie naye anachohitaji.

Usafi ni muhimu kila mmoja wetu.Kuoga kwetu ni usafi,kufua nguo zetu ni usafi,kufagia ni usafi pia.Hvy Leo nataka tujikite ktk mafunzo ya utengenezaji wa sabuni ya unga kwa ajili ya mahitaji ya kufulia nguo zetu na mahitaji mengineyo yahusuyo usafi.

Twende pamoja hapa chini.
UTENGENEZAJI WA SABUNI YA UNGA.

(1)MAANDALIZI:
(a)Beseni
(b)Mwiko
(c)Kijiko

(2)MALIGHAFI:
(a)Maji
(b)Sulphonic acid
(c)Sodash
(d)Sodium
(e)Silcate
(f)Nansa
(g)Optical-braytina.
(h)Perfume
(j)Rangi.(Blue wax).

(3)HATUA ZA UTENGENEZAJI:
(a)Pima maji safi Lita 1 tia kwenye Beseni safi.
(b)Pima sulphonic acid Lita 1 na nusu.
Anza kuimimina kwenye beseni lenye maji huku ukikoroga hadi sulphonic acid ijichanganye vizuri katika maji.
(c)Chukua silcate grasi 1 tia kwenye mchanganyiko huo.
(d)Chukua nansa na upime vijiko 5 weka katika mchanganyiko wako na ukoroge tena.
(e)Pima optical braytina vijiko 5 weka katika mchanganyiko wako kisha koroga tena mchanganyiko huo.
(f)Pima sodash kilo 6 weka katika mchanganyiko wako.
(g)Chukua sodium kisha pima kilogram 4,weka katika mchanganyiko wako.
(h)Chukua perfume na upime vijiko 4,weka katika mchanganyiko wako.
(j)Chukua rangi(Blue wax)kisha mimina katika mchanganyiko wako.
Baada ya hapo bila kupoteza muda anza kukoroga ama kuchanganya vizuri mchanganyiko wako kwa kutumia mwiko hadi mchanganyiko huo uwe raini kabisa.

Baada ya hapo anika sehemu safi kivulini.Na ni vizuri ukaianika sebleni ama chumbani palipo pasafi na pakavu..

Baada ya masaa 24,Sabuni yako ya unga itakuwa tayari kwa matumizi ya nyumbani kwako ama kwa biashara.
Weka sabuni yako katka vifungashio,weka lebo yako tayari kwa biashara.Na sabuni yako itakuwa na uwezo wa kudumu mwaka 1 bila kuharibika..

Kujifunza zaidi kwa vitendo,video na picha huna budi kuwasiliana nasi
+255746677970
+255629114323
+255625887699

Ahsante.

Jumanne, 3 Julai 2018

JIFUNZE KUTENGENEZA VIATU VYA KIMAASAI.

UJASIRI NI MALI(JIAJIRI).
Viatu vya Culture maarufu km viatu vya Kimaasai ni hitaji kubwa sana kwa watu hasa ukanda wetu huu Afrika Mashariki.Ni viatu pendwa mno na huvaliwa watu rika na jinsia zote.
Mahitaji ya viatu hivi yanaonekana kuwa makubwa hasa kutokana na ukwel kwmb,kwanza hamchoshi mvaaji,havina wakati wala mahala pa kuvivalia,huvaliwa na mtu yeyote kwa rangi yoyote ya nguo.Huvaliwa na kumpendeza kila anayeamua kuviavaa iwe kwa kushindia ama kwa kutokea.
Pili huuzwa gharama nafuu na hudumu muda mrefu iwapo utavinunua vikiwa bora,imara na kutunzwa vizuri.

Historia inaonesha kwmb viatu hivi vilianzakutengenezwa nchini Rwanda na hatimaye kuenea zaidi kanda ya Kaskazini mwa Tanzania vikiletwa na watu wa Kenya.
Viatu hv vilipewa jina la "Viatu vya Kimaasai",kwa sababu vinauzwa sana na jamii ya Wamaasai hasa nchini Tanzania...,na watu wengi hudhani ama kuamini kwmb Wamaasai ndiyo watengenezaji wa viatu hivi lkn ukwel ni kwamba Viatu hv havitengenezwi na Wamaasai na km wapo basi ni wachache sana.Badala yake viatu hv hutengezwa na watu wengine kabisa na Wamaasai wao ndiyo huvilangua kwa bei za jumla na kuanza kuvitembeza sehemu mbalimbali wakiviuza.Hvy kutokana na mara nyingi na sehemu nyingi unakutana na Wamaasai ndiyo wanaoviuza viatu hivi basi ndiyo maana likaja jina la viatu vya Kimaasai na ikakaririwa hivyo.

NINI FAIDA YA VIATU HIVI KWA MTENGENEZAJI.
Yah zipo faida nyingi sana kwa yeyote atakayeamua kuwekeza ktk mradi ama fursa hii ya viatu.
(1)Hukupa uhakika wa kipato muda wote utakapokuwa ukijihusisha navyo(kuvitengeneza).
(2)Hukutambulisha vema mbele ya wajasiriamali wengine,wachuuzi,wafanyabiashara wa viatu na mavazi,wateja wa rejareja na mataasisi mengineyo hasa ya mikopo mambo mengine kibao ya ujasiriamal na uwekezaji.
(3)Mwanzo wa kumiliki biashara yako na kiwanda chako binafsi.
(4)Unawezakuwa mwajiri mpya wa wengine hasa vijana na ukaisaidia serikali ktk kupunguza wimbi la watu wasiyo na ajira coz wapo watakaoajiriwa nawe kiwandani direct na lkn pia wapo watakaojiajiri wenyewe kwa kulangua mzigo kwako na wao wakaenda kuuza kwa watumiaji.
(5)Utaweza kuyamudu maisha yako ya kila cku kutokana na kupata kipato binafsi na chenye uhuru wa kukiamulia matumizi.
(6)Utatimiza malengo yako,ndoto na maono yako vile utakavyo mwnyw.
(7)Utajivunia kuwa mzalendo kwa kutumia malighaf za ndani ya nchi yako,ukazalisha na hvy utalipa kodi kwa ajili ya maendeleo ya Taifa lako.

SOKO LIKOJE?.
Ndiyo,
Soko la bidhaa hii lipo na ni kubwa tena lisilo na ukomo wa muda coz kila cku watu huvaa na hutaka wapendeze.Ikumbukwe kuwa viatu si sawa na nguo.

Mtu anaweza chanikiwa na nguo lkn akaishona ama akadumu nayo hata miaka miwili hadi mitatu lkn viatu huwa ni hitaji la kila cku.
Mtu hawezi katikiwa na kiatu mbele za watu na akamudu kutembea peku ilihali muuza viatu upo jirani tofauti na nguo.
Hvy soko lipo.Viatu hv unawezauza kwa jumla ama rejareja kwa mifumo utakayoiona ww kuwa inafaa.
Wapo wateja wanaonunua na kwenda kuvikopesha kwa watu wao huko majumbani,wengine hununua na kwenda kuviuza kupitia maduka yao ya nguo na viatu,wengine hununua na kwenda kuvichuuza minadani,magulio ama kutembeza mitaani na lkn pia wapo ambao huvinunua na kuvivaa wao binafsi.
Viatu hv pia vimeanza kuingizwa mataifa mengine ya nje ya Afrika Mashariki kutokana na wageni wengi wanaoingia na kutoka ktk ukanda huu pale wanapokutana navyo wakavinunua na kuvivaa wameonekana wakipendeza sana na pia hata wanapowachukulia na kuwapelekea wapendwa wao huko ktk mataifa yao bado vimeonekana kuwapendeza na kuwatia hamasa ya kuona kuna umuhimu wa kuvichukuwa huku Afrika na kuvipeleka kwao.

Mfano binafsi mnamo mwezi wa nne 2018 niliuza vuatu pea 32 vikaenda nchini Finland na aliyevipeleka aliwasiliana nami kwa Email kwmb aliviuza kwa muda mfupi sana na kwa pesa nzuri baada ya kuvifikisha kule.Akiahidi akiwa anarejea nchini Tanzania atanijuza nimtengenezee mzigo mwingine mkubwa na mzuri zaidi.
Hvy hii inaonesha ni jinsi gani kitu kidogo kwetu kinavyochukuliwa uzito mkubwa kwa wenzetu.

Hii ni fursa,idake,ikamate sawasawa,itafakari,ichanganue,ifanyie tafiti za kutosha na uchuwe hatua zaidi kuifanyia kazi..

KUNA AINA NGAPI ZA VIATU HIVI?
Yap,
Zipo aina kama 7 hivi za viatu hivi vya Culture(Kimaasai)
(1)Viatu vya ngozi pure
(2)Viatu vya ngozi yenye manyoya
(3)Viatu vya kitambaa
(4)Viatu vya Shanga kawaida
(5)Viatu vya shanga makirikiri
(6)Viatu vya shwapa/leather
(7)Viatu vya kufumwa kwa nyuzi.

Aina hizo 7 hutokana utofauti wa kimwonekano,ubora na matumizi ya malighafi tofauti tofauti zitumikazo kuvitengeneza viatu kulingana na eidha mahitaji ya soko ama mapendekezo(mapenzi)ya fundi tu mwenyewe.

UPATIKANAJI WA MALIGHAFI NA VIFAA UPOJE?
Twende kazi.
Aise upatikanaji wa malighafi hapa nchini Tanzania siyo mkubwa sana hasa kwa mikoa iliyo mbali na Arusha  ama kanda ya kati.
Lkn kwa mikoa km Arusha,Mwanza,Dodoma,Mbeya,Morogoro,Tanga na Dar es Saalam malighafi hizi zipo isipokuwa siyo kwa uwazi na wepesi sana km ilivyo sukari,chumvi ama unga kwny maduka mbalimbali kutokana na watumiaji wa malighafi zenyewe kuwa siyo wengi,yaani wanaojihusisha na utengenezaji wa viatu hivi siyo wengi mno.Hvy ili kuzipata inakulazimu kuulizia hasa kwa mafundi wa kushona viatu(Shoe shiners) wao watakuonesha ni wapi hununulia mahitaji yao hasa soli za kurepair viatu,kiwi,uzi nk kwani wanakonunulia vitu hivyo ndiko na malighafi hizi hupatikana ingawa siyo kwa mikoa yote km nilvyoeleza hapo juu.

Kuhusu vifaa pia vipo ktk maduka ya vifaa ya magari,mashine,ushonaji,ujenzi na maduka ya wajasiriamali wa bidhaa hii ya viatu.
Vifaa hivi ni pamoja na
>>Nyundo
>>Mikasi
>>Plaizi
>>Kinoo(Jiwe la kunolea)
>>Kisu(Patasi)
>>Purnch numbers
>>Purnch za kutobolea matundu
>>Magongo(Miguu bandia)
>>Size za miguu
>>Rula
>>Kalamu maalum(Silver pen)
>>Sindano
Nk.

Malighafi ni km vile
>>Gundi
>>Soli
>>Bango(box)
>>Shwapa/leather
>>Kitambaa(Valvet)
>>Kisigino(top up)
>>Pipe(Bomba)
>>Kamba(gidam)
>>Ribit
>>Michoro ya maua
>>Dawa(Leather clear na Dai)
>>Rubber band(vifungashio).

Naomba niishie hapa kwa leo.
Usisite kunifuatilia hapa hapa ktk chimbo lako la nguvu mnyausiblog.blogspot.com.
Au tembelea instagram jina Joachim Mkwawa.
Email:joachimmkwawa8@gmail.com
Au whatsapp namba +255629108340
Piga 0629114323/0746677970.

Ili ujifunze zaidi namna kutengeneza pesa kuputia fursa hii kwa kulipia ada kidogo tu itakayokupa kipato cha uhakika maishani mwako.

NB
UJASIRI NI MALI(JIAJIRI).
©Joachim L Mkwawa
New Vision with Common Skills.
Dodoma Tanzania