Jumamosi, 20 Oktoba 2018

Yanga yaiua Alliance Sports Club goli 3 kwa sifuri hii leo uwanja wa Taifa jijini Dar es Saalam.

Mchezo huo uliyokuwa wa vuta nikuvute ikishuhudiwa vijana wa Alliance kujaribu mara kadhaa kuliandama lango la Yanga,lakini hata hivyo juhudi hizo hazikuzaa matunda ambapo mnamo dakika ya 17 ya mchezo H.Makambo aliiipatia Yanga goli la kwanza,huku winga machachali Mrisho Khaphan Ngasa akifunga goli la pili mnamo dakika ya 29 ya mchezo kabla ya mapumziko.Na baadaye kipindi chapili Ibrahim Ajibu Migomba akamaliza kazi kwa kuipatia Yanga goli la 3 dakika ya 86 ya mchezo.

Hadi dakika 90 za mchezo Yanga 3 na Alliance 0

Hakuna maoni: