Ngara Kagera;
Mtoto wa mwaka mmoja aliyetupwa kwenye shimo La Choo cha wasichana shule ya msingi wilayani Ngara mkoani Kagera hatimaye ameokolewa.
Oparesheni hiyo ya uokozi ilifanywa kikamilifu na kufanikishwa kwa Ufanisi mkubwa wa Jeshi La Zimamoto na Uokoaji nchini Tanzania.Jeshi La Zimamoto nchini baada ya kupokea taarifa za tukio hilo La kusikitisha lilifika haraka eneo La tukio na kuanza kazi ya uokoaji mara moja na kufanikiwa kunusuru uhai wa mtoto huyo kwa kumtoa ndani ya shimo kupitia chemba(mfuniko)wa kalo La choo hicho.
Askari wa Jeshi La Zimamoto Constable Denis Minja alizama shimoni humo kwa kamba na kwa ujasiri na ufanisi mkubwa akiongozwa na Jeshi hilo alifanikiwa kumuokoa mtoto huyo ambaye kwa kipindi chote alisikika akilia ndani ya shimo hilo.
Kwa ujasiri huo pekee na wa kizalendo hatimaye Kamishina Jenerali wa Jeshi La Zimamoto na Uokoaji nchini Ndugu John Masunga akaamua kumpandisha cheo askari Denis Minja kutoka kuwa Constable hadi cheo cha Koplo.
Sisi kama jamii kwanza tunalipongeza Jeshi letu La Zimamoto na Uokoaji nchini kwa kutimiza vema wajibu wao wa kizalendo katika kushugulikia jambo hilo.Lakini pia tunalaani vitendo viovu na vya kinyama kama hivi vya watu(wazazi/walezi)kuchukua sheria mkononi na kutekeleza matukio yasiyo ya kibinadamu kama haya.Sambamba na kuwaasa Watanzania kuwa na hofu ya Mungu na kwamba ni kosa kisheria kutishia ama kukatisha uhai wa wengine kinyume na sheria zetu nzuri na bora zinazompa Mtanzania Uhuru na haki ya kuishi kwani kwa kufanyaje hivyo ni kupoteza nguvu kazi ya kesho kwa Jamii na Taifa kwa ujumla.
Mtoto wa mwaka mmoja aliyetupwa kwenye shimo La Choo cha wasichana shule ya msingi wilayani Ngara mkoani Kagera hatimaye ameokolewa.
Oparesheni hiyo ya uokozi ilifanywa kikamilifu na kufanikishwa kwa Ufanisi mkubwa wa Jeshi La Zimamoto na Uokoaji nchini Tanzania.Jeshi La Zimamoto nchini baada ya kupokea taarifa za tukio hilo La kusikitisha lilifika haraka eneo La tukio na kuanza kazi ya uokoaji mara moja na kufanikiwa kunusuru uhai wa mtoto huyo kwa kumtoa ndani ya shimo kupitia chemba(mfuniko)wa kalo La choo hicho.
Askari wa Jeshi La Zimamoto Constable Denis Minja alizama shimoni humo kwa kamba na kwa ujasiri na ufanisi mkubwa akiongozwa na Jeshi hilo alifanikiwa kumuokoa mtoto huyo ambaye kwa kipindi chote alisikika akilia ndani ya shimo hilo.
Kwa ujasiri huo pekee na wa kizalendo hatimaye Kamishina Jenerali wa Jeshi La Zimamoto na Uokoaji nchini Ndugu John Masunga akaamua kumpandisha cheo askari Denis Minja kutoka kuwa Constable hadi cheo cha Koplo.
Sisi kama jamii kwanza tunalipongeza Jeshi letu La Zimamoto na Uokoaji nchini kwa kutimiza vema wajibu wao wa kizalendo katika kushugulikia jambo hilo.Lakini pia tunalaani vitendo viovu na vya kinyama kama hivi vya watu(wazazi/walezi)kuchukua sheria mkononi na kutekeleza matukio yasiyo ya kibinadamu kama haya.Sambamba na kuwaasa Watanzania kuwa na hofu ya Mungu na kwamba ni kosa kisheria kutishia ama kukatisha uhai wa wengine kinyume na sheria zetu nzuri na bora zinazompa Mtanzania Uhuru na haki ya kuishi kwani kwa kufanyaje hivyo ni kupoteza nguvu kazi ya kesho kwa Jamii na Taifa kwa ujumla.